• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • M.M.M |
    • Barua pepe |
BUKOMBE DISTRICT COUNCIL
BUKOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Utumishi
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Kilimo na Umwagiliaji
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Idara ya Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Mifugo na Uvuvi
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu,Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC MURAGILI AWATAKA WANANCHI WAENDELEE KUSHIRIKI KATIKA MIRADI YA MAENDELEO

Imewekwa: April 16th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Eng. Paskasi Muragili amewataka Wananchi wa Kata ya Katome kuendelea kushiriki katika utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo.

Muragili ameyasema hayo tarehe 16 April 2024 alipokuwa anazungumza na Wananchi wa Kata ya Katome wakati wa ziara yake ya kusikiliza kero za Wananchi na kukagua Miradi mbalimbali ya Maendeleo.

Wakati wa Ziara hiyo Mhe. Muragili ametembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Katome iliyopo katika kijiji cha Miyenze ambayo imejengwa kwa nguvu za Wananchi ambapo hadi sasa ujenzi huo umegharimu kiasi cha Shilingi 13,946,000/=

 “Hongereni sana Wananchi wa Kata ya Katome na endeleeni kushiriki nguvu kazi katika ujenzi wa Miradi kwa ajili ya Maendeleo yenu”

 Vilevile Muragili alitembelea na kukagua mradi wa Ujenzi wa barabara ya Ntagalo-Kona 4-Miyenze yenye urefu wa kilomita 6.90 na barabara ya Miyenze-Butinzya yenye urefu wa Kilomita 6.31 na ujenzi wa kalvati laini 8 kwenye barabara ya Ntagalo-Kona 4-Miyenze na kalvati laini 18 kwenye barabara ya Miyenze-Butinzya.

Aidha Muragili amemtaka muhandisi wa TARURA kuhakikisha ujenzi wa barabara hiyo unakamilika kwa wakati ili kupunguza adha kwa wananchi katika kusafirisha mazao yao.

 “Ongezeni kasi katika ujenzi wa barabara hii ili ikamilike kwa wakati uliokusudiwa”

 Kwa upande wake diwani wa Kata ya Katome Mhe. Joseph Maganga ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kufanikisha ujenzi wa barabara hiyo Kwani imefungua shughuli za maendeleo kiuchumi.

Katika Ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya ameongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya, Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na wakuu wa Taasisi mbalimbali za Umma ikiwa ni muendelezo wa ziara yake katika Kata mbalimbali za Wilaya ya Bukombe.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10 February 10, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 23, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO YA 10% October 07, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC MURAGILI AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE ROBO YA TATU (Januari-Machi 2024/2025)

    May 08, 2025
  • WANANCHI WAJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 05, 2025
  • DC MURAGILI AHAKIKI TAARIFA ZAKE KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 05, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI MKOA WA GEITA.

    May 02, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkutano wa baraza la madiwani kwa kipindi cha robo ya 3 kwa mwaka 2024/2025
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mfumo wa Bajeti(Planrep)
  • Mfumo wa Fedha Vituo vya kutoa huduma(FFARS)
  • MTUHA
  • Maktaba ya Picha
  • Ramani ya Bukombe
  • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Ushirombo

    Sanduku la Posta: S.L.P 02

    Simu ya Mezani: 028 2520704

    Simu ya mkononi: +255 (0) 622 295619

    Barua Pepe: ded@bukombedc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • M.M.M
    • Mpangilo wa Tovuti
    • Service

Hatimiliki(c) 2017 Halmashauri ya Bukombe. Haki zote zimehifadhiwa