• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • M.M.M |
    • Barua pepe |
BUKOMBE DISTRICT COUNCIL
BUKOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Utumishi
      • Idara ya Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Kilimo na Umwagiliaji
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Idara ya Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi na Zimamoto
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Nyuki
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Mifugo na Uvuvi
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu,Afya na Maji
      • Kamati ya Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba
      • Ratiba ya Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
      • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Taasisi za Kidini Zatakiwa Kushirikiana na Serikali Kutokomeza Ukatili Nchini

Imewekwa: July 10th, 2022

Waziri wa madini mhe, Dkt. Dotto Biteko amewataka waumini wa kanisa la africa Inland Church Tanzania (AICT) dayosisi ya kalangalala Mkoani Geita kuiombea nchi pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Samia Suluhu Hassan Kwani nchi haiwezi kusimama bila maombi ya watakatifu pamoja na waumini wa dini mbalimbali.

Mhe, Dkt. Dotto Biteko ametoa Rai hiyo leo tarehe 10.7.2022 mkoani Geita wakati wa hafra ya uwekaji wakfu katika kanisa la africa Inland Church Tanzania (AICT Kalangalala) amesema watanzania kwa ujumla wanapaswa kuiombea nchi ili iwe na amani na usalama.

Waziri Dkt. Biteko amesema waamini wanapaswa kuliheshimu kanisa ikiwa ni pamoja na kufata sheria na kanuni za kanisa amewataka pia wazazi kuwafunza watoto kumpenda mungu ili wakue na maadili mema kwa lengo la kujenga taifa bora la kesho.

Amesema watoto wakilelewa katika misingi ya dini itawawezesha kukuwa vyema nakuwafanya wasijihusishe na mambo maovu ikiwemo matumizi ya madawa ya kulevya, wizi na mambo mengine ya kidunia.

Waziri Biteko ametumia nafasi hiyo kuzitaka pia taasisi za kidini nchini kuisaidia serikali kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa watoto unaondelea kushamiri kwenye maeneo tofauti hapa nchini.

Askofu Mkuu wa AICT, Askofu Mussa Magwesela amewataka wakazi wa Geita na Tanzania kwa ujumla kujitoa katika shughuli mbalimbali za kanisa kuunga mkono ujenzi wa nyumba za ibaada kwani zina mchango mkubwa katika kuimarisha maadili na kupiga vita vitendo viovu.

Amesema nyumba za ibada zikitumika vyema kuielimisha jamii juu ya maswala ya ukatili wa kijinsia zinanafi kubwa katika kuchangia kukemea maovu ambayo yanatokea katika jamii pamoja na kuchangia kuleta amani kwa jamii.

Naye Mbunge wa Jimbo la Geita mjini, Mhe Constantine Kanyasu amekiri kuwa endapo viongozi wa dini watasimama imara katika kukemea ukatili ndani ya mkoa wa Geita na maeneo mengine wataweza kuishinda vita dhidi ya ukatili.

Amesema ni Kweli hivi kalibuni kumekuwa na Matukio ya ukatili na matukio mengi yanahusianishwa na imani za kishirikina ameziomba taasisi za kidini kutoka nje makanisa kwajili ya kwenda kuwahubilia wananchi ambao bado hawamjui mungu kwani kufanya hivyo kutapunguza matukio ya ukatili katika jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO YA ASILIMIA 10 February 10, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 23, 2024
  • TANGAZO LA MIKOPO YA 10% October 07, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI September 16, 2024
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • DC MURAGILI AONGOZA KIKAO CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE ROBO YA TATU (Januari-Machi 2024/2025)

    May 08, 2025
  • WANANCHI WAJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 05, 2025
  • DC MURAGILI AHAKIKI TAARIFA ZAKE KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA

    May 05, 2025
  • MAADHIMISHO YA MEI MOSI MKOA WA GEITA.

    May 02, 2025
  • Tazama zote

Video

Mkutano wa baraza la madiwani kwa kipindi cha robo ya 3 kwa mwaka 2024/2025
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mfumo wa Bajeti(Planrep)
  • Mfumo wa Fedha Vituo vya kutoa huduma(FFARS)
  • MTUHA
  • Maktaba ya Picha
  • Ramani ya Bukombe
  • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara

Tovuti Muhimu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu(NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Ushirombo

    Sanduku la Posta: S.L.P 02

    Simu ya Mezani: 028 2520704

    Simu ya mkononi: +255 (0) 622 295619

    Barua Pepe: ded@bukombedc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • M.M.M
    • Mpangilo wa Tovuti
    • Service

Hatimiliki(c) 2017 Halmashauri ya Bukombe. Haki zote zimehifadhiwa